Saturday, June 22, 2013

WEMA SEPETU NA KAJALA MASANJA KIMENUKA...!!


Utabiri wa wengi kuwa ushosti wa waigizaji masistaduu wa Bongo Movies, Wema Isaac Sepetu na Kajala Masanja kutumbukia nyongo unadaiwa kutimia na sasa wametibuana, 

 “Walishinda wote, walilala wote, walikwenda klabu wote yaani Kajala alikuwa anamnyenyekea ‘madam’ Wema kwa kumuepusha na kifungo cha miaka 7 jela,” kilisema chanzo chetu na kuongeza:
 

“Kuna wakati hapa katikati Kajala alikuwa kama katibu muhtasi wa madam, si unajua lazima atumikie fedha za watu?

“Kabla hajaenda Mwanza kwa ajili ya mapumziko kwa bibi zake, nilimsikia Kajala akilalama kuwa madam aliamka siku moja akawa amemchunia, unaambiwa hata salamu ikawa hakuna.

“Hapo ndipo maneno ya pembeni yakaanza kwa sababu mbali na Kajala, Wema pia ana wapambe wengine na mbali na Wema, Kajala naye ana kampani. Kwa hiyo sosi ya manenomaneno ni hizo kampani zao.
 
“Ipo siku kabisa Wema alimlalamikia Kajala hadharani kuwa amekuwa akimsema vibaya kwa watu.
 
“Yale maneno yalimuuma sana Kajala, ikabidi arudi nyumbani kwao lakini akawa anaogopa kumwambia mama yake kuwa ametibuana na Wema hadi alipotimkia Mwanza.

“Lakini kabla ya hii ishu ya kulaumiana, kipindi cha nyuma kidogo Kajala alipata dili la kwenda kurekodi filamu nchini China na mastaa wengine lakini ikadaiwa kuwa Wema alichomoa hivyo mwigizaji huyo hakwenda pamoja na kwamba alishapewa baraka zote na baba yake.
 
“Unaambiwa alikuwa amekamilisha taratibu zote za kwenda China, hadi tiketi alikuwa ameshakata lakini suala hilo lilipotua kwa Wema, ilidaiwa kuwa alikataa kumruhusu.


TATIZO MILIONI 13?
“Mimi nakwambia zile milioni 13 zinamkosesha raha Kajala hadi unamuona kabisa kwamba ana stress (msongo wa mawazo).
“Wewe fikiria, kazi inayomwingizia mkwanja ni filamu, sasa unaambiwa inadaiwa kuwa madam hataki acheze filamu za watu wengine, sasa ataishije jamani?
 
 

“Mimi nakwambia ndiyo maana ameamua kwenda kupumzika Mwanza baada ya kuwa wananuniana kwa kwenda mbele.”

Baada ya kupata habari hizo, mwandishi wetu alimtafuta Wema kwa njia ya kilongalonga chake cha kiganjani ili kupata undani wa sakata hilo lakini hakupatikana hewani.

Baadaye mwanahabari wetu alisaga lami hadi kwa staa huyo Kijitonyama, Dar, alipogonga geti alitoka mlinzi aliyedai kuwa ‘malkia’ alikuwa ndani amelala na hakuhitaji usumbufu pamoja na kwamba ilikuwa saa 6:30 mchana.


Hata hivyo, mwanahabari wetu alibisha hodi ofisini kwa Wema, Mwananyamala-Komakoma ili kuzungumza na meneja wake, Martin Kadinda ambaye alikuwa na haya ya kusema:

“Ni kweli Kajala yupo Mwanza, aliomba ruhusa ya kwenda kupumzika tukampa. Hayo mengine ya kutibuana na madam siwezi kuyasemea kwa sababu yapo nje ya uwezo wangu.
 
 
“Lingekuwa ni suala la kazi hapo sawa lakini ni vizuri ukazungumza na mkurugenzi mwenyewe (Wema) lakini sidhani kama ataweza kuzungumza kwa sababu alikuwa anaumwa, amezidiwa na kupelekwa hospitali.”

Alipoulizwa Wema anaumwa nini, Kadinda alifunguka: “Sijajua lakini ugonjwa ni siri kati ya mhusika na daktari, cha msingi wewe ujue tu anaumwa.”

Baada ya kupita kote huko kusaka undani wa sakata hilo, mwandishi  alimgeukia Kajala kwa njia ya simu ya mkononi akiwa jijini Mwanza na kumuuliza kulikoni kutibuana na Wema.

Huku sauti ikiwa chini, Kajala alisema: “Ni kweli kuna hali ambayo hata mimi mwenyewe nashindwa kuelewa lakini siwezi kuzungumzia kwa leo nikiamini yatapita.”

Chanzo: Gazeti la Ijumaa

MSANII BARNABA WA THT AFIWA NA MAMA YAKE MZAZI..!!

Mwimbaji kutoka Tanzania House of Talent (THT) Barnabas Elias maarufu kama Barnaba amefiwa na mama yake mzazi alfajiri ya leo jijini Dar es salaam.

Taarifa zilizothibitishwa na rafiki wa karibu na msanii mwenzake Amini , zinasema mama yake Barnaba amefariki nyumbani kwake alfajiri ya leo Jumamosi (June 22) kutokana na presha.

Monday, June 17, 2013

STEPS FILM AWARDS 2012-13 Steps film awards 2012-13 was held at Blue Pearl Hotel Dar Es Salaam on 15/06/2013. Honorable Minister for communication, science and Technology Prof.Makame M.Mbarawa inagurated the function officially . Thanks for all the Artists , Delegates , Corporates , Media ,Special Guests , Bongo Movie Viewers, Well wishers & Colleagues for your Great Support .









STEPS AWARDS 2012-13
1.Best Director : Ray Kigozi (Women Of Principle)
2.Best Actor: Jacob Steven ( Nakwenda Kwa Mwanangu )
3.Best Actress : Iree Paul
4.Best Movie : - Kijiji Cha Tambua Haki 
5.Best Selling Movie :- Ndoa Yangu
6..Best Best Story :- Nice Muhammed (Baamed)
7.Best Screen Play :- Ally Yakuti
8.Best Cameraman :- Zakayo Magulu
9.Best Sound :- Bharghasi Saidi
10.Best Editor : Timoth Conrady
11.Best Production House:RJ Production Company
12.Best Supporting Actor : Rado (I think I hate my wife )
13.Best Supporting Actress: Riama Ally ( Tabu Ya kuolewana)
14.Best Producer : John Lister
15.Best Comedian :King Majuto
16.Most Promising Actor : Niva
17.Most Promising Actress : Irene Paul
18.Best Child Artist : Jennifer
19.Best Action Movie :Double J
20.Best Perfomance in a negative role : Mohammed Nurdin -checkbudi (Azma)
21.Special Jury Award : Jennifer Kyaka (odama) 
21.Best movie on National Integration:Mwalimu Nyerere 
22.Best Movie for the development of culture & Language :Toba
23.Posthumous Awards :- Late:Kanumba, Late:Sajuki , Late:Sharobaro,Late:John

Friday, June 14, 2013

PICHA :ENZI HIZO KUNDI LA WAKILISHA LILILOUNDWA NA SHAA,WITNESS NA LANGA KABLA HAWAJATENGANA


R.I.P LANGA KILEO....!!!


Kilichosemwa na hospitali ya Muhimbili kuhusu kifo cha msanii Langa.



Aminiel Aligaesha ambae ni Afisa Uhusiano wa hospitali ya Taifa Muhimbili amethibitisha kwamba msanii Langa amefariki dunia June 13 2013 saa kumi na moja jioni baada ya kufikishwa hospitalini hapo toka juzi jioni ambapo kutokana na sababu za kimaadili kwenye tiba, Muhimbili hospitali hawawezi kusema rapper huyu alikua anaumwa nini bali ndugu ndio wenye mamlaka ya kufanya hivyo.
Kwenye maelezo aliyoyatoa kwa millardayo.com Aminiel amesema Marehemu Langa alipokelewa kwenye idara ya wagonjwa wa magonjwa ya dharura usiku wa kuamkia jana na kupatiwa huduma ambapo leo June 13 2013 ndio alihamishiwa kwenye chumba cha wagonjwa Mahututi na baadae kufariki dunia.

Thursday, June 13, 2013

STEPS KUANZA KUTOA TUZO KWA WASANII WAKE WA FILAMU

 
Meneja Masoko wa Steps Entertainment, Kambarage Ignnatus akionyesha moja ya tuzo zitakaotolewa kwa wasanii sikuya Jumamosi kwenye ukumbi wa Blue Pearl, Ubungo Plaza, kulia ni  Mwakilishi wa kampuni ya Steps Solar, Johnson Mwamba.Na Mwandishi Wetu

Kampuni ya usambazaji wa filamu Tanzania ya Steps Entertainment limited Jumamosi  itatoa tuzo kwa wasanii, Watayarishaji, Waongozaji, na wadau mbalimbali waliopo katika tasnia ya filamu Tanzania.
Mratibu wa tuzo hizo, Carlos Johns Silondwa alisema kuwa tuzo hizo zitafanyika kwenye ukumbi wa Blue Pearl Ubungo Plaza na zitawahusisha zaidi wasanii wanaofanya kazi na kampuni yao tu.
Silondwa alisema kuwa kutakuwa na vipengele nane ikiwa pamoja na Filamu Bora ya Mwaka, Kampuni iliyotengeneza filabu bora, msanii anayependwa na watu ndani na nje ya mwisho, msanii bora chipukizi, muigizaji bora wa kike, muigizaji bora wa kiume, muongozaji bora wa filamu na mwandishi bora wa filamu.
Silondwa alisema kuwa wameandaa tuzo hizo kwa lengo la kuanzisha tuzo hizo ni kuleta ushindani na kukubali mchango wa wasanii, watayarishaji na wadau wote kampuni inatumia fursa hii ya kuwatambua na kujali mchango wa wasanii katika ukuzaji wa filamu nchini Tuzo ni kichocheo kitakacholeta ushindani unaoweza kujenga tasnia ya filamu na kujenga ajira kwa jamii kubwa.
Alisema kuwa tuzo hizo zimezingatia michango mbalimbali kutoka kwa wadau mbalimbali ambao wamekuwa mbele katika kutangaza tasnia ya filamu ndani na nje ya nchi kupitia njia mbalimbali, pia kutakuwa na tuzo za heshima kwa waliotangulia kuitambulisha tasnia ya filam u Tanzania.
“Tunaamini kuwa tuzo zitakuwa kichocheo kikubwa cha kukuza tasnia ya filamu kuongeza ushindani katika kutengeneza filamu Bora, hadithi nzuri zinazoelimisha, kukuza na kuitangaza lugha ya Kiswahili nje ya mipaka ya Tanzania lugha ambayo imekuwa ikukua kila siku kwa kupitia filamu za kitanzania zinazopenyeza na kuvuka mipaka ya nchi,” alisema Silondwa.
Alisema kuwa wanaarajia kuwa na Tuzo kubwa zitakazoshirikisha wadau wote kwa baadae, na kuwa ni moja kati ya moja ya kampuni wadhamini wa tuzo zenye mlengo wa kimataifa, mwaka huu kampuni imeandaa tuzo hizo pasipo kuwatumia wadhamini wa nje ya kampuni ikipata udhamini kwa kampuni ya Steps Solar pekee



Mwakilishi wa kampuni ya Steps Solar, Johnson Mwamba (mwenye koti) akizungumzia udhamini wa kampuni yao katika tuzo za Steps Movie Award zilizopangwakufanyika Jumamosi kwenye ukumbi wa Blue Pearl.